VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

21 Novemba 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Kiongozi wa Mungiki aachiwa huru

23/10/2009

Angry members of the Luo tribe carry another Luo after he was attacked by a Kikuyu crowd during ethnic clashes in the central Kenyan town of Nakuru, 25 Jan 2008
Kiongozi wa kundi lililopigwa marufuku nchini Kenya la Mungiki, Maina Njenga, ameachiwa huru Ijumaa baada ya kuwa kizuizini kwa muda mrefu kutokana na shutuma za kukabiliwa na makosa ya mauaji.

Serikali ya Kenya kupitia mwanasheria mkuu ilisimamisha kesi dhidi ya kiongozi huyo ambaye amekuwa akipambana kortini kufuatia mashtaka ya mauaji yaliyokuwa yakimkabili.

Kiongozi huyo wa kundi la Mungiki alikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya watu 29 ambapo maafisa wa polisi walidai mauaji hayo yalifanywa na wafuasi wa kundi lake kufuatia agizo la kiongozi huyo. Mara baada ya kuachiwa huru kiongozi huyo alisema ana furaha na sasa anataka mwanzo mpya wa maisha bora.

Viongozi wa kitengo cha kisiasa cha Mungiki-Kenya National Youth Alliance, wakiongozwa na Njuguna Gitau wameunga mkono kuachiliwa huru kwa kiongozi huyo.


Download Kenya Mungiki
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Kenya Mungiki
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mapya

  Mahojiano zaidi