VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

21 Novemba 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Kampeni za uchaguzi mkuu Msumbiji za pamba moto

26/10/2009

Electoral campaign in Tete, North of Mozambique
Kampeni ya uchaguzi Tete, kaskazini ya Msumbiji
Wagombea kiti cha urais nchini Msumbiji wamefanya kampeni zao za mwisho kabla ya upigaji kura siku ya Jumatano. Wagombea wote watatu walimaliza kampeni zao Jumapili, wakiwasihi wafuasi wao kujitokeza kupiga kura.
 
Uchaguzi unatarajiwa kumpatia ushindi Rais Armando Guebuza, ambaye anakabiliana na mgawanyiko wa upinzani. Wapinzani wake ni Afonso Dhlakama, kiongozi mkuu wa chama cha upinzani cha Renamo, na Daviz Simango, mwanzilishi wa chama kilichojitenga cha Democratic Movement of Mozambique.

Simango alijitoa kutoka chama cha Renamo mwanzoni mwa mwaka huu, na kuwachukua maafisa wakuu wa upinzani. Upigaji kura wa Jumatano utachagua pia viongozi wa bunge na majimbo.
 
Chama tawala cha Frelimo kimeongoza Msumbiji tangu ilipopata uhuru wake kutoka Ureno mwaka wa 1975.


 

 


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya

  Mahojiano zaidi