VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

21 Novemba 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Marekani yaiwekea Sudan vikwazo

28/10/2009

US President Barack Obama delivers major speech on finacial crisis at Federal Hall in New York, 14 Sep 2009
Rais wa Marekani Barack Obama.
Rais wa Marekani Barack Obama ameweka upya vikwazo dhidi ya Sudan, akisema hatua za serikali ya nchi hiyo zinaendelea kuwa kitisho cha usalama kwa nchi ya Marekani.
 
Vikwazo hivyo vinadhibiti biashara na uwekezaji baina ya Marekani na Sudan, na pia vinalenga marufuku ya kusafiri na kuzuia mali, za baadhi ya maafisa wakuu wa Sudan.
 
Rais Obama alisema angeweka upya vikwazo hivyo, alipotangaza sera mpya za utawala wake kwa Sudan wiki iliyopita. Sera hizo mpya kwa Khartoum zinalenga kuishinikiza serikali hiyo kuongeza juhudi za kuleta amani, na kuionya kuwa itakabiliwa na shinikizo zaidi kutoka kwa Marekani endapo hatazingatia hilo.
 
Marekani inataka kuona mzozo wa Darfur umetatuliwa pamoja na utekelezaji kamili wa mkataba wa amani uliofikiwa baina ya Kaskazini na Kusini, na kuhakikisha Sudan haitakuwa maficho ya magaidi wa kimataifa.

 


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya

  Mahojiano zaidi