VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

21 Novemba 2009 

Leo VOA:

Habari katika Lugha 45
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni

10/11/2009

kenya flag 150 site eng.jpg
Bendera ya Kenya.
Jopo la wataalamu nchini Kenya wanaotathimini marekebisho ya katiba nchini humo, tayari wameandika kielelezo ambacho kinatarajiwa kuchapishwa na baadaye kujadiliwa katika juhudi za kuandaa katiba mpya ya Kenya. Mapendekezo hayo ni pamoja na kupunguzwa kwa madaraka ya rais, kuwepo kwa waziri mkuu mwenye madaraka ya kiutendaji na bunge lenye mabaraza mawili.

Wataalam wa maswala ya katiba na wachambuzi wa habari wanasema hiyo ni hatua kubwa katika juhudi za kuipatia Kenya katiba mpya, lakini wanatahadharisha kwamba bado kuna kazi kubwa ya kufanywa kufanikisha zoezi hilo. Sauti ya Amerika imezungumza na wakili wa masuala ya sheria P.L.O Lumumba na kumuuliza mapendekezo yaliyomo katika kielelezo hicho.

 


Download Katiba Kenya
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Katiba Kenya
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya

  Mahojiano zaidi