Somalia Yakanusha Kuingia tena Majeshi ya Ethiopia
21/05/2009
Wapiganaji wa Kiislam nchini Somalia
Ripoti kutoka Somalia zinasema wanajeshi wa Ethiopia wamerudi nchini humo kujaribu kurejesha hali ya usalama baada ya waasi wa nchi hiyo kuzidisha mashambulizi katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
Lakini Waziri wa Habari wa Somalia Farhan Ali Mohamud anasema serekali imesikia ripoti hizo kutoka vyombo vya
habari kuwa majeshi ya Ethopia yameingia lakini anasema hadhani ni ripoti
sahihi.
Hatahivyo alisema inaeleweka kwa Ethopia kupeleka wanajeshi
wake kwenye mpaka kujilinda kutokana na kuendelea kwa vita i upande wa pili wa
mpaka ndani ya Somalia.
Majeshi
ya Ethopia yaliondoka mwezi Januari mwaka huu baada ya makubaliano ya amani
kufikiwa kati ya serekali na kundi la Rais Sharif Sheikh Ahmed katika upinzani, lakini Ethopia ilisema majeshi yatarudi ikiwa maslahi yake yako hatarini.
Ethopia ina kikosi kikubwa
cha wanajeshi kwenye mpaka wake. Serekali ya Ethopia imekanusha kwamba
wanajeshi wake wameingia nchini humo. Tangu May 8 wanaharakati kutoka makundi
ya al-Shabab na Hizbul Islam, mungano wa wanamgambo wamekua wakipambana na
majeshi ya serekali na wanamgambo wanaoiunga mkono serekali na majeshi ya
kulinda amani ya Umoja wa Afrika.