VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Raila: Uongozi Mbaya Unachelewesha Maendeleo Afrika


26/05/2009

Raila Odinga (file photo)
Akiongea na Sauti ya Amerika muda mfupi kabla ya kutoa hotuba yake katika chuo kikuu cha Buffalo, New York, Waziri Mkuu Odinga alisema kuwa mfumo mbaya wa uongozi umewanyima Waafrika haki ya kupanga namna ya kujiletea maendeleo yao wenyewe. 

Bwana Odinga alisema kuwa Afrika inahitaji mabadiliko yatakayo saidia kupunguza mamlaka kupita kiasi yaliyowekwa katika taasisi za urais. Alisema hili litasaidia kuondokana na mifumo ya kidikteta, na kuingia mfumo wa uongozi wa kidemokrasia utakao wapatia mamlaka wananchi. 

Akizungumza kuhusu suala la rushwa na mvutano wa kisiasa katika serikali ya mseto ya Kenya, Waziri Mkuu Odinga alisema kuwa tayari kuna maendeleo yaliyo patikana tangu ilipoundwa serikali ya mseto. 

Hatahivyo, Bwana Odinga alikiri kuwa kumekuwepo na matatizo kadhaa katika serikali hiyo, lakini pia akasema mabadiliko tayari yanafanyika. 

Alitoa mfano wa tume mpya ya uchaguzi ambayo imeundwa hivi karibuni, na kwamba Kenya iko katika harakati za kuunda tume ya ukweli, kaki na maridhiano itakayo saidia kuponya vidonda vilivyo patikana wakati wa machafuko yaliyofuatia uchaguzi wa nchi hiyo.


Download Odinga-US-Africa
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Odinga-US-Africa
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available