VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Wakenya Wazomea Hotuba ya Rais Kibaki


01/06/2009

Tanin and his herd of cows
Uchumi wa Kenya
Hotuba ya Rais Mwai Kibaki wa Kenya ilikatishwa kwa kelele za wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa kuadhimisha miaka 46 tangu nchi hiyo ilipojipatia uhuru wake wa ndani. 

Katika hali ya kuashiria kuwa hawaridhishwi na jinsi mambo yanavyo endelea nchini Kenya, wananchi walipiga kelele kumzomea Rais Kibaki pale alipokuwa akijaribu kuelezea mafanikio yaliyofikiwa nchini humo, na mikakati ya serikali yake kwa siku za baadaye. 

Sarah Nyamvula ni mtetezi wa haki za mama na mtoto nchini Kenya. Anasema licha ya kwamba wakenya walijipatia utawala wao binafsi miaka 46 iliyopita, bado kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za watoto, kina mama na binadamu wote kwa ujumla. 

Naye mchambuzi wa siasa Maur Bwanamaka alisema kuwa Kenya imeharibika kwa sababu viongozi wa kisiasa wanazingatia zaidi malumbano ya kisiasa, na kwamba mwananchi wa Kenya bado anaendelea kunyanyasika licha ya kujipatia uhuru wake wa ndani miaka 46 iliyopita.


Download Kenya Madaraka
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Kenya Madaraka
Sikiliza (MP3)
Download Madaraka-Uchambuzi
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Madaraka-Uchambuzi
Sikiliza (MP3)
Download Madaraka-Maoni
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Madaraka-Maoni
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available