VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Rais Omar Bongo yuaga dunia

08/06/2009

Rais omar Bongo alifariki akiwa na umri wa miaka 73 baada ya kugua kwa muda katika zahanati moja huko Barcelona, Hispania, kutokana na kile serekali ya Gabon inaeleza ni "mshtuko mkubwa" kufuatia kifo cha mkewe mwezi March mwaka huu.
Gabon President Omar Bongo (2006 file photo)
Rais Omar Bongo wa Gabon

Kifo chake na ugonjwa wake hapo kabla zilizusha ripoti za kutatanisha, ambapo vyombo vya habari viliripoti awali kwamba amelazwa hospitali akiwa mahtut kutokana na ugonjwa wa saratani ya tenzi kibofu, serekali ikikanusha. Na shirika la habari la Ufaransa liliporipoti kifo chake Jumapili tarehe 7 June serekali ikakanusha. 

Rais Bongo alichukua madaraka 1967 akiwa wakati huo kiongozi kijana kabisa aktika bara la Afrika. Alichukua madaraka baada ya kifo cha rais Leon M'ba aliyefariki miaka 7 baada ya kuchukua madaraka kutoka ukoloni wa Ufransa. 

Wakati wote wa utawala wake alijaribu kua mpatanishi wa migogoro ya nchi mbali mbali ya afrika ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Afrika ya Kati, Burundi , Na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongol. Lakini Gabon ilikua nchi ya pili ya Afrika iliyotambua uhuru wa walotaka kujitenga huko Biafra nchini Nigeria. 

Kiongozi huyo wa muda mrefu, aliyesilimu mwaka 1973 na kubadilisha jina lake la Albert Bernad Bongo na kua Omar Bongo, alikubali mfumo wa vyama vingi mwaka 1990, lakini aliendelea kutumia utawala wa mabavu hadi kufariki kwake.

Yeye ni mmoja kati ya viongozi watatu wa Afrika wanaofanyiwa uchunguzi na jaji mmoja wa Ufaransa kwa mashtaka ya ulaji rushwa na utumiaji mbaya wa fedha za umaa. Shirika la kimataifa la kupambana na ulaji rushwa Tranparency International inadia zaidi ya nyumba na majengo ya familia ya Bongo huko Ufarnsa yanthamani ya zaidi ya dola milioni 200.


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available