VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Ghailani adai Mahakamani NY, "Sina Hatia"

09/06/2009

Maafisa wa wizara ya sheria ya Marekani wamemwasilishwa Mtanzania Ahmed Khalfan Ghailani mbele ya mahakama ya serekali kuu mjini New York na kufunguliwa mashtaka kwa kuhuiska kwake katika uripuaji wa mabomu kwenye ubalozi wa Marekani huko Kenya na Tanzania 1998. 

aptn pakistan al qaida Ahmed Khalfan Ghailani on FBI poster eng 150 2aug04.jpg
Ahmed Khalifa Ghailani mfungwa wa Guantanamo
Bw Ghailani alikamatwa nchini Pakistan mwaka 2004 na kuhamishwa na wafungwa wengine mwaka 2006 walotaja kua ni "wafungwa muhimu sana." 

Maafisa wa wizara ya sheria wamefikisha mashtaka 286 dhidi ya Bw Ghailani ikiwa ni pamoja na kupanga njama pamoja na Osama Bin Laden na wanachama wengine wa al-Qaida ili kuwauwa Wamarekani, pamoja na mashtaka binafsi ya mauwaji ya kila aliyefariki katika mashambuliyo hayo ya mabomu.

Bw Ghailani amedai mbele ya hakimu kwamba hana hatia kufatana na tuhuma hizo zote.

Bw Ghailani ni mfungwa wa kwanza wa Guantanamo kufikishwa mbele ya mahakama ya kiraia hapa Marekani. Kesi yake inatazamiwa kua mtihani wa kwanza muhimu kwa mpango wa Rais Barack Obama wa kulifunga gereza la Guantanamo mnamo miezi saba ijayo, na kuwafikisha wafungwa mahakamani.


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available