VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Hali Iran haitabiriki kwa sasa


15/06/2009

Supporters of reformist presidential candidate Mir Hossein Mousavi carry his poster, during a rally in Azadi street in Tehran, 15 June 2009
Wafuasi wa kiongozi wa upinzani Mir Hossein Mousavi wakiandamana mjini Tehran.

Rais wa Marekani Barack Obama amekariri wasiwasi wake juu ya matukio nchini Iran kufuatia matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyozusha ubishi na kusababisha maandamano katika mitaa na barabara za mji mkuu Tehran.

Akizungumza na sauti ya Amerika Jumatatu mchambuzi wa maswala ya kisiasa Profesa Xavery Lwaitama alisema maandamano yanayoonekana Tehran yanatokana na vijana na watu wanaotaka mabadiliko.

 Alisema waandamanaji hao wangependa kuwa huru kutumia vyombo vya habari vya kisasa. Profesa Lwaitama alisema taifa la Iran limejikita katika misingi ya kidini na kwamba ushawishi wa nchi za magharibi huenda umechochea azma ya kuyataka mabadiliko.

Akizungumza kuhusu rais Mahmoud Ahmadinejad aliyechaguliwa kwa muhula wa pili, mhadhiri huyo wa chuo kikuu cha Dar-es-Salaam Tanzania, alielezea kuwa rais Ahmadinejad ana uungaji mkono wa viongozi wa wengi wa kidini akiwemo Ayatollah Ali Khamenei na kwamba anajionyesha kuwa mtu wa kawaida. 

Profesa Lwaitama alisema huenda mpinzani wake Mir Hossein Mousavi amepigwa na mshangao  sasa kwamba amewasha moto wa kisiasa asioweza kuzima kwa kupinga matokeo ya uchaguzi huo, na kwamba litakaloibuka baada ya ghasia hizi haliwezi kutabiriwa.         


Download Hali Iran haitabiriki kwa sasa
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Hali Iran haitabiriki kwa sasa
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available