VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Waislamu Kenya walaani ugaidi

22/06/2009

Ciidamada Al-Shabaab
 Al-Shabaab
Kufuatia kuibuka kwa makundi ya kigaidi nchini Somalia na Kenya. Serikali ya Kenya imeanza kuchunguza madai kuwa vijana wanaanza kuandikishwa kujiunga na kundi la kigaidi la Somalia Al-Shabaab.

Lakini nchini Kenya, inaripotiwa mkenya kwa jina Saleh Ali Saleh Nabhan anaongoza kundi lake la kigaidi lenye ushirika na mtandao wa kigaidi wa al Qaida kwa jina Al-Muhajirun. Kundi lake hilo yaripotiwa lina wapiganaji waliopewa mafunzo nchini Afghanistan na Pakistan.

Akizungumza na sauti ya Amerika kutoka Mombasa, mwenyekiti wa baraza kuu la mashauri la waislam wa Kenya Sheikh Juma Ngao, alisema viongozi wa dini ya kiislam wanajiandaa kutoa hamasa kwa waislamu kote nchini humo kupitia misikiti na madrassa kuwaelezea vijana misingi na nguzo za dini ya kiislam ambayo inalaani vikali vitendo vyote vya kigaidi.

Aidha Sheikh Ngao alisema hivi karibuni baraza lake litaanda kukutana na familia ya Saleh Nabhan kusikiliza maoni yao na kutoa ushauri kwao kufutia tendo la kijana huyo kujihusisha na vitendo vya kigaidi. Nabhan anatuhumiwa kuhusika na jaribio la kutungua ndege ya Israel ikiwa katika anga ya Kenya na hoteli ya Paradise mjini Mombasa .

Na kuhusu ombi la Somalia kuzitaka nchi jirani za Kenya, Djibouti, Ethiopia na Yemen kupeleka majeshi yao kusaidia serikali dhaifu ya Somalia, Sheikh Ngao alisema haungi mkono ombi hilo. Alisema kupeleka majeshi hayo nchini Somalia ni kuhatarisha maisha yao bure na kwamba tatizo la kisiasa la Somalia linapaswa kutatuliwa na wasomalia wenyewe, kwani ni watu wa kabila moja, lugha moja na dini moja.


Download Viongozi wa kidini walani ugaidi
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Viongozi wa kidini walani ugaidi
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala zaidi
Somalia Yakanusha Kuingia tena Majeshi ya Ethiopia
 
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available