VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Wabunge wa Somalia wakimbilia Kenya

24/06/2009

 Mapigano yanayongozwa na wanaharakati wakislamu wenye itikadi kali yamewapelekea wabunge 15 wa Somalia  kukimbilia nchi jirani ya Kenya, wakihofia maisha yao. 

Wabunge hao  waliwasili Nairobi mapema wiki hii wakisema hali ni ya hatari na hawaamini serikali ya mpito inaweza kuendelea kupambana na vikosi vya wanamgambo wa al-Shabab na washirika wao bila ya msaada wa kigeni.

Kuna zaidi ya wabunge 280 walobaki huko Mogadishu ili kuhakikisha miswada inapitishwa, kwani inahitajika wabunge 250 kati ya wabunge 550 wa bunge la mpito kuweza kuwa na majadiliano yeyote.

A Somali man carries a boy wounded during mortar shelling, 17 Jun 2009, in Mogadishu
Mtoto aliyejeruhiwa kwa mzinga anabebwa na mtu moja huko Mogadishu
Wakati huo huo mwandishi wa Sauti ya Amerika Mwai Gikonyo, anaripoti kwamba zaidi ya watu 100 waliojeruhiwa vibaya kutokana na majeraha ya risasi, waliwasili Nairobi na kupelekwa katika hospitali mbali mbali za mji huo wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Balozi wa Somalia mjini Nairobi Bw Ali Noor, amesema hospitali za Mogadishu zimeja majeruhi na hazina uwezo wa kuwatibu watu waliojeruhiwa vibaya sana. Awali polisi wa Kenya waliwazuia majeruhi hao pamoja na wabunge kuingia nchini humo wakitoa sababu za kiusalama.

Lakini kibali kilitolewa baada ya Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR kuingilia kati na kuitaka Kenya kuheshimu sheria za kimataifa za kuwalinda majeruhi wa vita.


Download Kenya Somalia mps
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Kenya Somalia mps
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available