VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Michael Jackson akumbukwa kote duniani

26/06/2009

Mwana muziki mashuhuri kabisa wa muziki hapa Marekani Michael Jackson alifariki alhamisi tarehe 25 June baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo nyumbani kwake huko Los Angeles. Alikua na umri wa miaka 50 na ni mmoja kati ya wasanii waliokua maarufu sana duniani ambaye alichanganya pamoja muziki wa aina ya pop, rock na soul uliowavutia watu wengi duniani wa kila rangi na utamaduni.

Michael Jackson alizaliwa tarehe 19 Augusti 1958 mjini Gary, Indiana akiwa mtoto wa saba kati ya watoto tisa. Yeye na kakazake wanne wakubwa walionekana tangu wadogo wakiwa na kipaji cha muziki, kuimba na kucheza dansa na hasa kuhimizwa na wazazi wao. Akiwa na umri wa miaka mitano alishuka kwa mara ya kwanza katika jukwaa na kuanza kuimba pamoja na ndugu zake hao wakiuwa na kundi la Jackson Five.

In this 13 Nove 1988, file photo, pop singer Michael Jackson performs before a sold out crowd for his Bad tour at the Los Angeles Sports Arena
Michael Jackson huko Los Angeles Nov 13 1988.
Baada ya mashindano ya muziki katika ukumbi mashuhuri wa Apollo huko New York Jackson Five walitia saini mkataba wao wa kwanza na kampuni ya rekodi ya Motown, na kuanzia 1964 hadi 1981 kwa pamoja ndugu hao waliuza zaidi ya rekodi milioni 100.

Mbali ya kuwa msanii hodari, mfanya biashara na mtu mkarimu Michael alikumbwa na kashfa kadhaa katika maisha yake na kubwa ni tuhuma ya kuwanajisi watoto wadogo, jambo ambalo mahakama iliamua hakua na hatia. 

Kabla ya kufariki kwake, alikua anafanya mazoezi na matayarisho kwa ajili ya tamasha lake kubwa kabisa huko London la kutaka kurudi upya kwenye jukwaa la muziki na kuwaonyesha wakosowaji wake kwamba yungali ni mfalme wa pop. Lakini muda wake ulifika na aliaga dunia kwa ghafla kabisa. Mola amlaze pema Peponi.


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available