VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Ajali ya ndege Comoros

30/06/2009

Kiasi ya watu 152 wanahofiwa wamefariki kutokana na ajali ya ndege ya aina ya Airbus 310 ya shirika la ndege la Yemenia iliyoanguka kaskazini ya kisiwa cha Ngazija visiwani Comoros. 

Maafisa wa usfiri huko Comoros wanasema, ndege ilijaribu kutua kiasi ya saa tisa usiku lakini kutokana na upepo mkali na gurudumu moja la ndege kutoweza kushuka rubani alilazimika kuruka tena na hapo ndipo ajali ikatokea. 

Relative of passenger cries at Marseille airport, southern France, 30 Jun 2009
Jamaa za wathiriwa huko Marseille Ufransa June 30 2009
Mohamed Said Mchangama rais wa baraza la mameya wa Ngazija anasema hadi Jumanne usiku kulikua na hali ya mtafaruku kote nchini kwani kila mji kulikua na angalu mtu moja aliyekua abiria. Na hakuna aliyekua anajua kinachotendeka, hata hivyo ndege ya kijeshi ya Ufaransa ili kiwa na waokozi na madaktari imefika mchana wa leo na kuanza juhudi za kutafuta mili ya watu na mabaki ya ndege hiyo. 

Familia ya wathiriwa wameimabia sauti ya Marekani kwamba hawana habari zezote juu ya juhudi zinazoendelea isipokua nambari imetolewa kupiga kujua habari za jamaa zao, lakini imekua vigumu kabisa kupata habari zozote.


E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available