VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
Bakwata yapinga kutoundwa mahakama ya Ki-islam

02/07/2009

 

Kwa mujibu wa BAKWATA kikubwa wanachokitaa waislam ni kujumuisha sheria za kislam kwenye sheria za nchi.


Katika tamko lake juu ya kuundwa kwa mahakama ya kadhi lililotolewa bungeni, waziri wa sheria na katiba alisema tume iliyoundwa kushughulikia suala la kuwepo au kutokuwepo kwa mahakama ya kadhi imetaka kutafsiriwa baadhi ya sheria za kislam na kuzijumuisha katika sheria za nchi na sio kuundwa kwa mahakama ya ki-islamu.

Sheikh mkuu wa Tanzania Issa bin Shaban Simba, katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam Alhamisi terhe 2 Julai alisema, “waziri anasema amekutana na wataalam hatujui wataalam wale ni wataalam wa sheria za kislam au ni wataalam wa kawaida".


Aliendelea kusisitiza kwamba “isione kigegezi serikali kuanzisha mahakama ya kadhi nchi hii ina mahakama mengi, mahakama ya nyumba kuna mahakama ya kadhi kuna mahakama za bahari za sheria wala hatudai kwamba kuna siku waislam katika mahakama hizo watakata mkono mtu au wataua mtu kesi za jinai ni kesi za mahakama kuu ya serikali” .


Sheikh Shaban Simba anasema kwa upande wao cha muhimu ni kutaka kuhukumu masuala ya ndoa na mirathi mambo ambayo anasema yanapotoshwa kwa muda mrefu.

Sheikh mkuu alisema “waziri hakufafanua ni nani atasimamia nani tunalozungumza si sheria ya kislam kuwepo lakini nani msimamizi wa sheria hizo. Tumechoshwa waislam kupotoshwa mambo yetu”.

Kwa mantiki hiyo Sheikh mkuu wa Tanzania alisema baraza kuu la waislam wa Tanzania linapinga hatua hiyo.


 


Download Mahakama ya Ki-islam Tanzania
Fungua  (MP3)
Listen to This Report Mahakama ya Ki-islam Tanzania
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Marekani na India kuimarisha ushirikiano wao

  Mahojiano zaidi
Rais Umaru Yar'Dua wa Nigeria, kwenda Saudi Arabia kwa matibabu
Suala la Ardhi EAC Lafafanuliwa  Audio Clip Available
CUF yafurahishwa na hotuba ya Karume  Audio Clip Available
Israel na Misri zatoa mwito wa amani
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja  Audio Clip Available
Hatari ya gesi katika Ziwa Kivu  Audio Clip Available
Kielelezo cha Katiba Kenya Kujadiliwa  Audio Clip Available
Marais Obama na Hu wajadili uchumi kati ya Marekani na China
Umoja wa Mataifa waahidi kuteketeza baa la njaa duniani  Audio Clip Available
Wanawake watoa wito wa mabadiliko Zanzibar  Audio Clip Available
Mafuriko yaongezeka Tanzania  Audio Clip Available
Chama cha Bemba DRC chaelekea kugawanyika
Mapendekezo ya Katiba mpya Kenya kuchapishwa karibuni
WHO: wanawake wabaguliwa kupata huduma za afya
Miaka 20 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin
Chanjo ya Malaria Yakaribia  Audio Clip Available