VOANews.com

Sauti ya Amerika ▪ SwahiliPata habari za kuaminika

 
Habari katika Lugha 45
EAC yakubaliana juu ya soko la pamoja

20/11/2009

Traders gather in western Kenya for the fishing auction
Wafanya biashara wakusanyika magharibi ya Kenya

Marais wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki wanaokutana Arusha,Tanzania kuadhimisha miaka 10 ya umoja huo wametia saini mkataba wa soko la pamoja la nchi hizo na kuzindua mradi wa kutoa kompyuta za bure za mkononi - Laptop - kwa shule za msingi kutoka nchi wanachama wa jumuia hiyo. Mara baada ya mkataba huo kutiwa saini viongozi wa taasisi na wakuu mbali mbali wa biashara nchini Tanzania, wametoa maoni mbali mbali kuhusu faida ya soko la pamoja.

\Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko wa Tanzania, Sirel Chami, aliwataka wa-Tanzania kuongeza ubora wa bidhaa zao wanazozalisha ili kukidhi haja ya soko hilo la pamoja.
 
Amesema “kama una kiwanda chako na unaajiri watu 500, sasa unaweza ukaajiri watu elfu mbili” kwa hiyo unaweza ukajenga ajira zaidi kwa wa-Tanzania kwa sababu soko limepanuka. Vile vile unachangia zaidi katika pato la Taifa kwa sababu utalipa kodi kubwa zaidi na unapolipa kodi kubwa zaidi inamaanisha kwamba Taifa litakuwa na uwezo zaidi wa kuboresha huduma za barabara, shule, maji na sekta nyingine ambazo zinahitajika nchini humo.
 
Kwa upande wa sekta binafsi serikali ya Tanzania inasema imeshaanza kuwaandaa wafanyabiashara wa Tanzania ili kuweza kumudu ushindani katika taratibu mpya za soko la pamoja katika nchi tano husika za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.  
 


Download EAC mkataba
Fungua  (MP3)
Listen to This Report EAC mkataba
Sikiliza (MP3)
E-mail This Article Mtumie rafiki makala
Print This Article Chapisha bila picha
  Makala mepya
Nigeria yakasirishwa na matamshi ya Gadhafi

  Mahojiano zaidi
Obama ahimiza kupitisha mswada wa mageuzi ya afya.
Mahakama ya kimataifa yapinga rufaa ya Bikindi
Ghasia za kidini zaibuka tena Nigeria
AU ina wawekea vikwazo viongozi wa Madagascar
Jacob Zuma awasili Zimbabwe kutatua mzozo wa kisiasa
Wataalamu wa ukimwi eneo la IGAD wakutana Kenya  Audio Clip Available
Wabunge Kenya wamtaka Mudavadi ajiuzulu  Audio Clip Available
Wakimbizi wengi wa Sudan wamerudi nyumbani
Kenya na Congo zatajwa katika ripoti ya haki za binadamu  Audio Clip Available
Ukarabati wa barabara ya Uganda na Rwanda waanza
Tahadhari yatolewa kuhusu uchaguzi Sudan
Afisa wa Marekani aomba msamaha kwa Libya
Bill Gates Ashuka Daraja katika Utajiri
Wakazi laki tano kuhamishwa Uganda
Baadhi ya maeneo Burundi yakumbwa na njaa  Audio Clip Available
Matukio ya Upigaji majumbani yaongezeka Kenya
Wakenya Wataka majina 20 ICC yafichuliwe  Audio Clip Available
Uganda yaongoza EA katika orodha ya FIFA
Sarkozy Akiri Makosa ya Ufaransa