Sauti ya Amerika ▪ Swahili
Pata habari za kuaminika

Kwa Maandishi Pekee
Search

Hawa ni watangazaji wako ambao umekua ukiwasikia kwenye matangazo ya Sauti ya Amerika.

 

Mwamoyo Hamaza

Mwamoyo Hamza     

Mwamoyo Hamza ni mtangazaji mwandamizi katika Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika. Mzaliwa wa Tanga, Tanzania, Mwamoyo alisomea uandishi
habari katika Chuo Cha Uandishi wa Habari cha Dar es Salaam, Tanzania na baadaye shahada za juu katika chuo kikuu cha Howard mjini Washington D.C. Alijiunga na VOA mwaka 1994. Mbali na vipindi vya habari Mwamoyo pia anatayarisha makala za kila wiki za "Amerika Leo" na "Kilimo Wiki Hii."


Abdushakur Aboud

Abdushakur Aboud
 

Abdushakur ni mtangazaji wa muda mrefu aliyejiunga na VOA 1992. Yeye ni mzaliwa Zanzibar lakini anatokea visiwani Comoro. Alihetimu uandishi habarim katika chuo kikuu cha Dakar, Senegal, na kupata mafunzo ya utangazaji wa Televisheni huko Ujerumani na Japan. Alifanyakazi na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani, na baadae idhaa ya kiswahili na kingereza ya redio ya UIngereza BBC. Hivi sasa hutayarisha vipindi vya televisheni vya VOA pamoja na vipindi vya "Masuali na Majibu" na Muziki kutoka Afrika."


Ester Githui Ewart

Esther Githui Ewart

Esther Githui Ewart  ni mtangazaji katika idhaa ya Kiswahili  na televisheni ya Sauti ya Amerika . Ni mzaliwa Kenya ambaye alisomea uandishi habari katika chuo kikuu cha Nairobi. Kabla ya kujiunga na Chuo hicho alisomea shahada ya elimu katika chuo kikuu cha Kenyatta na kufundisha  kwa muda mfupi katika shule mbalimbali za sekondari nchini Kenya . Anafahamika vyema nchini humo ambapo kwa muda wa miaka minane aliandaa vipindi na kusoma taarifa za habari katika shirika la kitaifa la  televisheni na radio - K.B.C. Esther alijiunga na  Sauti ya Amerika  mwaka  2000. Mbali na kazi za kila siku za kuandaa ripoti na taarifa za habari, ni mhariri na mwandalizi wa kipindi kinachopendwa  sana “Jarida la Jumapili” ambapo huwaletea mahojiano ya kina  ya kijamii, kisiasa  kiuchumi na kitamaduni akiwaalika washiriki mbalimbali kutoka maeneo ya Afrika ya Mashariki; ya kati, Marekani na kwingineko . Amewahoji maafisa wakuu wa  serikali ya Marekani juu ya sera ya Marekani kwa Afrika mkiwemo  rais George W. Bush mwaka wa 2002 katika ikulu ya White House,  Seneta Barack Obama wa jimbo la Illinois, mbunge Maxine Waters wa California miongoni mwa wengine. Kwa starehe zake  Esther anapenda kupumzika na  familia yake,  kusoma na kufuatilia matukio mbalimbali kupitia  vituo vya  televisheni.


  

Khajida Riyami

Khadija Riyami 

Khadija Riyami alijiunga na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika mwaka 1998. Kabla ya hapo alikuwa ni Mhariri wa Michezo katika magazeti ya Daily News/Sunday News nchini Tanzania.  Pia aliwahi kuwa mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani - Deutschewell na mwandishi wa kipindi cha michezo cha Fast Track katika Shirika la Utangazaji la Uingereza - BBC. Khadija hivi sasa ni Mhariri na pia anaandaa vipindi vya Dunia ya Wanawake na Matukio ya Afrika. alipata shahada ya uandishi kutoka Chuo cha waandishi wa habari nchini Tanzania na kupata mafunzo ya juu ya uandishi nchini Afrika Kusini, Ujerumani na Uingereza.